Posti Maarufu

Thursday, November 11, 2010

WALIMU WA SAUT WANAWALAZIMISHA WANAFUNZI WA KIKE KUFANYA NAO NGONO LA SIVYO .

Hii ni Barua iliyo tumwa kwa VC na DVCAA wa SAUT KUHUSU UDHALILISHAJI WA WANAFUNZI HASA WA MWAKA WA KWANZA

Ndugu,
'Maadili' au 'uadilifu'  ni Msingi  mkubwa sana katika Kuboresha Elimu na Kuwajenga Wataalamu wenye Maadili na Uadilifu ili kuweza kulinjenga taifa letu hili lililonyuma kimaendeleo. Ili Kupata Wahitimu walio na Maadili mema na waadilifu  katika kulitumikia taifa ni vema Wakufunzi wa Vyuo wawe na Maadili mema na Waadilifu.

Wazazi Wanapowaruhusu watoto wao kuja Vyuoni... wanakuwana IMANI Kubwa sana na Wakufunzi ,kwamba wataendeleza Malezi na Maadili mema ambayo wazazi wamewafundisha watoto wao. Miaka ya Nyuma Mwanafunzi mmoja aliandika Makala katika Gazeti la Familia, inayohusu 'Jinsi  Wakufunzi wanavyowadhalilisha Watoto wa kike katika Vyuo Vikuu wakitishia Kuwafelisha iwapo hawatakubali kufanya nao Mapenzi'. Kwa bahati mbaya Gazeti hilo lilipotea baada ya Muda mfupi na halikuendelea kuchapishwa.. Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu ikakaa kimya labda kwa kuwa hawakuweza kulisoma..... Mimi ninayo nakala ya Makala hiyo.
Baada ya Hapo mimi pamoja na Wadau wengine wa Mapambano ya Udhalilishwaji na Unyanyasaji dhidi ya Wanawake tulianza kufanya Utafiti kuhusu hali hiyo... Na baada ya Muda Mabinti wengi sana waliwasilisha malalamiko yao kwetu kuhusu Kuombwa Unyumba na Wakufunzi na kutishiwa kufelishwa mitihani iwapo hawatakubali.

Nichukue nafasi hii  Kwa niaba ya Timu ya Marafiki wa Maisha Tanzania kukufahamisha kuwa Hadi wiki iliyopita tumepokea Malalamiko Mengi sana ya Wanafunzi kutoka Katika Chuo Chako.
Malalamiko Mengi yanatoka kwa Vijana wa Mwaka wa Kwanza hasa wakiwalalamikia Wakufunzi Vijana. Mfano ni Mkufunzi wa somo la Sociology  katika Kampasi ya Mtwara ambaye ni kijana na hana Muda mrefu katika Kazi hii. Mkufunzi huyu amakuwa akiwasumbua wanafunzi kwa kuwaita ofisini na kuwatongoza huku akitishia kuwafelisha mitihani iwapo hawatamkubali..na bahati nzuri tunayo recording ya Manongezi yake na baadhi ya Wanafunzi wa kike.Tunayo pia malalamiko ya Wakufunzi wa BAED Katika Kampus ya Mwanza na Malalamiko mengine mengi tu

Natambua kuwa moja wapo ya Vigezo vya kuwachagua Wakufunzi vyuo vyenu ni kuwa lazima Mwombaji awe Mwadilifu na mwenye kufuata maadili ya Ualimu  na iwapo hazinagatii hili na kuwachagua wakufunzi kwa kuangalia vigezo vingine kama ujamaa na undungu (japo siamini kuwa mnafanya hivyo). Kama hiyo ndivyo ilivyo ninyi kama wakuu wa vyuo hivi mnalo jukumu la kusimamia maadili haya.
Jina la chuo ni Mtakatifu Agustiono, Maisha ya Mtakatifu huyu yalijaa uadilifu na ndiyo maana Vatikan ikaamua kumweka katika maisha ya Utakatifu.. Tulitegemea pia wakunfunzi wa Chuo wawe watakatifu kimaadili.
 Tukiangalia Mission na Vision yenu
VISION ya SAUT
When the Catholic Bishops of Tanzania decided to extend the Church’s services to the provision of higher education they envisioned a training that would not only impart academic and professional skills but also that would inculcate values of civic and social learning and ethics, such as acquisition of national identity, cultural norms, political growth and responsible citizenship. Thus the Church’s vision is the holistic development of a person and respect for human dignity.

St. Augustine University of Tanzania strives at:
  • being a centre of excellence by providing a high quality of education, research and public service;
  • promoting the pursuit and defence of truth with transparency and honesty, and service with competence and dedication;
  • developing a sense of caring for personal and community property;
  • a holistic development of the person by providing sound knowledge, higher analytical ability and commitment to generous service and respect for humankind.
  • Conscious of man’s orientation towards God and neighbour and fostering an ethical and service-oriented approach in its academic and professional training, St. Augustine University of Tanzania fulfils its goal by preparing persons well equipped to contribute to the ideals of social, economic and political development.
Iwapo Wakufunzi wenu ndiyo Chanzo cha kuvunja MISSION na VISION Zetu je Watanzania wataaminije kuwa Vision na Mission zenu ni za Kweli?
Kwa Kuanzia Tunawasilisha maombi kwenu hasa kumhamisha mkufunzi wa BAS kwa Mwaka wa Kwanza katika Kampus ya Mtwara. Kwa kuwa awali alikuwa na masomo matatu na sasa  ameachiwa masomo mawili baada ya kuletwa kwa  Mkufunzi mwingine.. Ni vema jukumu hilo akaachiwa mkufunzi huyu mgeni
Tunajua Kuna risk ya Kufelishwa Mitihani kwa Wanafunzi walioleta malalamiko yao lakini tumejiweka vizuri kupambana na hali hiyo ikiwa ni pamoja na kwenda mahakamani ili mitihani yao isahihishwe na wakufunzi watakaoteuliwa na mahakama (Iwapo watfelishwa na Mkufunzi huyu na ushahidi wa recordings na Picha tulizonazo zatosha kabisa.... Lakini tusingependa kufikia huko. Ni Vema uongozi wa chuo Uchukue hatua za haraka kuhakikisha kuwa wakufunzi wanakuwa na maadili na kwa kuwahamisha wale wanaolalamikiwa na kuwapa Maonyo.

Tunatarajia kuwa uongozi  wenu utachukua hatua  muafaka kutatua hali hii. Tunaendelea Pia Kuwasiliana na Cecylia Malamsha, Ass. Dean wa Mtwara Kampus ambaye hata hivyo bado hajatoa msaada sana pengine ni kwa sababu hana mamlaka ya kumhamisha Mkufunzi

Tutaendelea kuwapa taarifa za malalamiko ya Wanafunzi kwani lengo letu ni kuahikisha tunakuwa na vyuo vikuu vyenye maadili sahihi
Na tutatumia Mfumo wa Utoaji HAKI nchini ambayo ni Mahakama iwapo hamtachukua hatua za Haraka


Wenu Katika Udumishaji wa Maadili Nchini, 
M/Kiti
MTANDAO WA WADAU WA MAADILI NCHINI

1 comment:

  1. kuficha majina sio kujenga ni dalili za uoga. si mwadai kuwa na vielelezo andikeni majina yenu sasa. uhuni, TUJA na NJEMU tu mwafanya hapo.

    ReplyDelete