Mtandao wetu umepata taarifa kuwa Mkuu wa Deaprtment ya Procurement and Supplies Management katika chuo cha CBE Bwana Mohamed amekuwa akiwanyanyasa wasichana wa kike kwa makusudi.
Bwana Mohamed amekuwa akiwasumbua wasichana wa kike kwa kuwatongoza na Pindi wanapomkaa hujenga chuki dhidi yao na kutoa alama zisizo za haki katika Mitihani yao. Kutokana na Recordings tulizonazo za maongezi yake na Baadhi ya Wanafunzi wa kike waliowasilisha malalamiko yao kwetu,imedhihirika kabisa kuwa tabia ya Mkufunzi huyu haina Maadili.
Uchunguzi wa awali tulioufanya, umedhihirisha kuwa baadhi ya Wanafunzi Wamenyanyaswa katika mitihani kwa Makusudi na Mwalimu huyu. Tunauomba uongozi wa Chuo uchukue hatua za haraka.
Wazazi wanapowaleta watoto wao chuoni wana imani kuwa wakufunzi wataendeleza malezi mema yenye kuwajenga wanafunzi kimaadili ili kuzalisha wataalamu wenye maadili mema ya kulinjenga taifa letu na iwapo wakufunzi watakuwa ndio wa kwanza kuharibu maadili je wataalamu watakaozalishwa watakuwa na maadili gani? Na wazazi tutakuwa na imani gani dhidi ya Vyuo.
Iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa tutampleleka Mahakamani mkunfunzi huyu na kwa Ushahidi wa recordings na Picha tulizonazo itatosha kabisa kumuwajibisha mkufunzi huyu huku tukiomba Mahakama itoe kibali kwa Mitihani yote ya Wanafunzi walioferishwa isahihishwe na Mkufunzi wa nje atakayeteuliwa na Mahakama ili kudhihirisha Uonevu na Kuwalinda walioleta Malalamiko... Hatupendi kufika huko hivyo tunaamini uongozi wa CBE utachukua hatua muafaka ili kuepuka kuharibika kwa credibility ya Chuo kwa Jamii
Mwanamtanda
Huu ni Muungano wa Wanaharakati,Wanahabari,Wanasheria na Wananchi wa Kawaida wenye nia Njema ya Kurekebisha Maadili ya Watanzania. Hapa Utapata Habari kuhusu Uvunjwaji wa Maadili na Uonevu wa Makundi Maalumu ya Kijamii. Tuungane Kutokomeza Uonevu na Unyanyasaji dhidi ya Wasio weza Kujitetea wenyewe. Wasiliana nasi kwa barua pepe: uadilifu@yahoo.com
Posti Maarufu
-
VIONGOZI WA UMMA WALIOKO KATIKA ORODHA HII WAMEKIUKA NA/AU KUVUNJA MASHARTI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO (Kwa Hisani ya Website ya Chade...
-
Hii ni Barua iliyo tumwa kwa VC na DVCAA wa SAUT KUHUSU UDHALILISHAJI WA WANAFUNZI HASA WA MWAKA WA KWANZA Ndugu, 'Maadili' au ...
-
“………..nikiwa nimejipumzisha chumbani kwangu,chumba ambacho kipo mahali ambapo kwa lugha ya wenyewe tuyaita ‘Hostel’,ghafla mlango ulifunguli...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment