Posti Maarufu

Friday, November 12, 2010

MKUU HUYU WA DEPARTMENT YA PROCUREMENT AND SUPPLIES CBE ACHUKULIWE HATUA ZA KINIDHAMU

Mtandao wetu umepata taarifa kuwa Mkuu wa Deaprtment ya Procurement and Supplies Management katika chuo cha CBE Bwana Mohamed amekuwa akiwanyanyasa wasichana wa kike kwa makusudi.
Bwana Mohamed amekuwa akiwasumbua wasichana wa kike kwa kuwatongoza na Pindi wanapomkaa hujenga chuki dhidi yao na kutoa alama zisizo za haki katika Mitihani yao. Kutokana na Recordings tulizonazo za maongezi yake na Baadhi ya Wanafunzi wa kike waliowasilisha malalamiko yao kwetu,imedhihirika kabisa kuwa tabia ya Mkufunzi huyu haina Maadili.
Uchunguzi wa awali tulioufanya, umedhihirisha kuwa baadhi ya Wanafunzi Wamenyanyaswa katika mitihani  kwa Makusudi na Mwalimu huyu. Tunauomba uongozi wa Chuo uchukue hatua za haraka.
Wazazi wanapowaleta watoto wao chuoni wana imani kuwa wakufunzi wataendeleza malezi mema yenye kuwajenga wanafunzi kimaadili ili kuzalisha wataalamu wenye maadili mema ya kulinjenga taifa letu na iwapo wakufunzi watakuwa ndio wa kwanza kuharibu maadili je wataalamu watakaozalishwa watakuwa na maadili gani? Na wazazi tutakuwa na imani gani dhidi ya Vyuo.
Iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa tutampleleka Mahakamani mkunfunzi huyu na kwa Ushahidi wa recordings na Picha tulizonazo itatosha kabisa kumuwajibisha mkufunzi huyu huku tukiomba Mahakama itoe kibali kwa Mitihani yote ya Wanafunzi walioferishwa isahihishwe na Mkufunzi wa nje atakayeteuliwa na Mahakama ili kudhihirisha Uonevu na Kuwalinda walioleta Malalamiko... Hatupendi kufika huko hivyo tunaamini uongozi wa CBE utachukua hatua muafaka ili kuepuka kuharibika kwa credibility ya Chuo kwa Jamii


Mwanamtanda

No comments:

Post a Comment